Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ukarabati wa Stendi Kuu ya Mabasi Bweri iliyopo Manispaa ya Musoma?

Supplementary Question 1

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Kwa kuwa miradi ya TACTIC, imeshaanza na Halmashauri ya Manispaa ya Mji wa Musoma haimo kwenye miradi hiyo kwa sasa.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha mradi huo unaanza? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Stendi ya Mabasi ya Mji wa Musoma ina hudumia wananchi kutoka Tarime, Serengeti, Rorya, Butiama, Musoma Vijijini na maeneo mengine yanayozunguka Mkoa wa Mara. Kwa sasa stendi ile ni chakavu sana na haipitiki hasa mvua ikinyesha. Je, Serikali ina mkakati upi wa muda mfupi, kuhakikisha stendi ile inaendelea kuingilika ili kusubiri mkakati wa muda mrefu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ghati Zephania Chomete, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Miradi ya TACTIC, itaanza utekelezaji wake rasmi mwaka wa fedha 2022/2023, lakini Halmashauri hii ya Musoma pia ipo kati ya zile lot ya kwanza, ya pili na ya tatu ambapo tutakwenda kutekeleza. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba itapokuwa inaanza mwaka ujao wa fedha, basi Manispaa hii ya Musoma hii stendi itakuwa miongoni mwa zile lot tatu ambazo zipo kwenye TACTIC.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na Stendi ya Mabasi ya Musoma Mjini kuwa ni chakavu sana na inahudumia wananchi wengi. Natoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma kuhakikisha wanatenga fedha za mapato ya ndani, kwa sababu stendi ni kipaumbele lakini ni chanzo cha mapato. Kwa hiyo, lazima mapato ya ndani yaanze kuboresha stendi ile wakati wanaandaa andiko la kuomba fedha kama mradi wa mkakati kwa ajili ya kukamilisha. Ahsante.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ukarabati wa Stendi Kuu ya Mabasi Bweri iliyopo Manispaa ya Musoma?

Supplementary Question 2

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wananchi wa Mkoa wa Rukwa wanateseka sana kuhusiana na stendi, stendi iko mbali na stendi ya zamani iko mjini. Je, ni lini sasa Serikali itaruhusu wananchi wa Mkoa wa Rukwa watumie stendi zote mbili kama inavyotumia Mkoa wa Mbeya, wanashusha Uyole, wanashusha Nane Nane na wanashusha stendi ya zamani. Hivyo, ni lini sasa Serikali itaruhusu wananchi wa Rukwa watumie stendi ya zamani?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, maamuzi ya mkoa kwa maana ya Viongozi wa Mkoa; Mkuu wa Mkoa, Katibu Tawala na Menejimenti za Halmashauri zetu zote, nawaelekeza wakae wafanye tathmini kwamba kwa nini stendi ya zamani haitumiki na inatumika stendi mpya ambayo iko mbali na waone uwezekano wa kufanya maamuzi stendi ipi itumike au zitumike zote na watupe mrejesho Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Kwa hiyo, suala hilo litafanyiwa kazi na Serikali. Ahsante.

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ukarabati wa Stendi Kuu ya Mabasi Bweri iliyopo Manispaa ya Musoma?

Supplementary Question 3

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Ni muda mrefu sasa katika Mji wa Babati hatuna stendi na stendi haijamaliziwa. Je, ni lini Serikali italeta fedha ili ujenzi ule wa stendi ya Babati ukamilike kama ulivyoahidiwa? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Regina Qwaray, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa stendi na miradi mingine yote ya kimkakati, kwanza ni jukumu la halmashauri kuainisha gharama, lakini pia kuwasiliana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kuona kwanza kama wana uwezo wa kuzijenga kupitia mapato ya ndani, lakini pili kama wanahitaji kupata fedha kutoka Serikali. Kwa hiyo, mamlaka ya Halmashauri ya Babati, ilete taarifa ya mpango wa utekelezaji wa stendi ile ili Serikali tuone namna ya kufanya, kama watajenga kwa mapato ya ndani au kama tutafuta fedha kwa ajili ya kujenga kama mradi wa kimkakati. Ahsante.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ukarabati wa Stendi Kuu ya Mabasi Bweri iliyopo Manispaa ya Musoma?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa stendi ya mabasi ya Shinyanga Manispaa imechakaa na ni ya zamani haijajengwa kisasa, je, ni lini Serikali itajenga Stendi Kuu ya Mabasi, Manispaa ya Shinyanga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, stendi hizi zote kama nilivyotangulia kujibu kwenye jibu la awali la halmashauri husika, Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, wafanye tathmini na kuona gharama ambazo zinahitajika kukamilisha au kujenga stendi ile, lakini waone uwezo wao wa mapato ya ndani kutenga kwenye bajeti. Kama inahitaji gharama kubwa, walete andiko hilo Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ili tuweze kufanya tathmini na kutafuta vyanzo vya fedha. Ahsante.