Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Kata ya Kwihancha itapata Kituo cha Afya na ni lini huduma za afya zitaimarishwa katika Hospitali ya Nyamwaga?

Supplementary Question 1

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza ni kwamba, wakati wa bajeti tarehe 26 Machi, 2022 kwenye Kamati ya TAMISEMI, waliahidi wataalam kwamba watapeleka fedha hizi tarehe 30 Machi. Leo Waziri anasema tarehe 30 Mwezi Juni, maana yake miezi mitatu baadaye. Kama hii kauli ya mwanzo iliahidi Kamati ya Fedha, fedha haijaenda mpaka leo tunavyozungumza, tarehe 30 Juni, fedha itaenda kweli?

Swali la kwanza, fedha hiyo inaenda lini Ili iweze kujenga kituo cha afya pale? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; hapo Hospitali ya Mwaga ilikuwa ni zahanati kama kituo cha afya, sasa ni Hospitali ya Halmashauri mpya, hakuna mgao wa dawa pale, lakini hizi huduma ninazozizungumza wodi ya akinamama haijakamilika, wodi ya watoto haijakamilika, wodi ya wanaume haijakamilika, pharmacy haijakamilika, fedha ipo milioni 78 kwenye mgodi wa North Mara, Mheshimiwa Waziri wa Madini aliagiza kwamba ndani ya siku 14 fedha iende haijaenda, Waziri wa TAMISEMI aliagiza fedha haijaenda...

SPIKA: Mheshimiwa Mwita Waitara, ngoja kwanza. Jibu la msingi la Waziri, wewe kwa hilo swali lako la pili unalotaka kuuliza ni kwamba, hili jibu lake la msingi halitoi uhalisi wa kilichoko huko ndiyo unachojaribu kusema? Simama.

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ni kweli.

SPIKA: Kwa hiyo, hakuna hizo wodi mbili zilizokamilika.

MHE. MWITA M. WAITARA: Hazijakamilika.

SPIKA: Basi hilo swali lako la nyongeza la kwanza nitampa nafasi Mheshimiwa Waziri alijibu, hilo la pili unalosema hayo majibu hayako halisi Mheshimiwa Naibu Waziri atakapomaliza kujibu maswali hapa, nitampa nafasi aende akalifuatilie aniletee majibu hapa.

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Waitara, Mbunge wa Jimbo wa Tarime Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Halmashauri ya Tarime Vijijini walitakiwa kupeleka milioni 100 lakini hawakupeleka milioni 100 katika kata hii kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kituo cha afya tarehe 30 Machi na jana nimewasiliana na Mkurugenzi na Katibu Tawala wa Mkoa na watapeleka ndani ya mwezi huu kwa sababu walikuwa hawajapata makusanyo ya kutosha kupeleka fedha hiyo kwa mujibu wa vipaumbele ambavyo vilikuwa vimewekwa. Ahsante sana.

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Kata ya Kwihancha itapata Kituo cha Afya na ni lini huduma za afya zitaimarishwa katika Hospitali ya Nyamwaga?

Supplementary Question 2

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Lutende, mwaka 2019 walipeleka shilingi bilioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya na jengo la OPD limekamilika. Palikuwa pana ongezeko la milioni 300 lakini kata hiyo haijapelekewa fedha hiyo. Je, ni lini watapeleka fedha hiyo ili tuweze kumaliza Kituo cha Afya cha Kata ya Lutende?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nnaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kituo hiki kilipelekewa milioni 200 na kama ilivyo kwa vituo vyote ambavyo vilipelekewa milioni 200 au milioni 250, awamu inayofuata wanapewa milioni 300 au milioni 250 kukamilisha milioni 500 ili kukamilisha vituo vya afya. Kwa hiyo, fedha hiyo itapelekwa kwenye kituo hicho cha afya. Ahsante.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Kata ya Kwihancha itapata Kituo cha Afya na ni lini huduma za afya zitaimarishwa katika Hospitali ya Nyamwaga?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Miluwi iko umbali wa kilomita 80 kutoka Liwale Mjini ambako kuna hospitali ya wilaya na uhitaji wa kituo cha afya pale ni mkubwa sana na wananchi wameshaanza ujenzi wa kituo cha afya pale. Je, Serikali iko tayari kusaidia kwenye bajeti hii kuunga mkono juhudi zile za wananchi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza niwapongeze sana wananchi wa Kata hii ya Miluwi ambao wameanza kuchangia nguvu zao kujenga kituo cha afya na niwahakikishie kwamba Serikali itaendelea kuchangia katika hizo nguvu za wananchi ili kuhakikisha kwamba kituo hicho kinakamilika kwa awamu. Ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Kata ya Kwihancha itapata Kituo cha Afya na ni lini huduma za afya zitaimarishwa katika Hospitali ya Nyamwaga?

Supplementary Question 4

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Wananchi wa Kata ya Dalai walijihamisha wakaanza ujenzi wa kituo cha afya. Lini sasa Serikali nayo itaweka nguvu zao ili kituo kile kimalizike? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Jimbo la Chemba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa sababu wananchi wameanza ujenzi wa kituo cha afya kwa nguvu zao, tumewapongeza kwa juhudi hizo, lakini Serikali itaendelea kutafuta fedha kama ilivyo kwa majimbo mengine yote ili kuchangia nguvu za wananchi kukamilisha vituo ambavyo vimeanza ujenzi. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira kwamba Serikali inatambua hilo na italifanyia kazi. Ahsante.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Kata ya Kwihancha itapata Kituo cha Afya na ni lini huduma za afya zitaimarishwa katika Hospitali ya Nyamwaga?

Supplementary Question 5

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, ni lini Zahanati za Tandika pamoja na Mibulani zitaanza kufanya kazi kwa sababu majengo yako tayari na kila kitu na yameanza kupata ufa, tusiipoteze Serikali fedha zile. Je, ni lini zitaanza kufanya kazi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dorothy Kilave, Mbunge wa Jimbo la Temeke, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, vituo vyote vilivyokamilika vinatakiwa vianze kutoa huduma mapema iwezekanavyo na natoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke kuhakikisha zahanati au vituo hivi vya Tandika na Mibulani vinasajiliwa haraka iwezekanavyo na vinaanza kutoa huduma kwa wananchi kama ilivyotarajiwa.