Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, kuna mango gani wa kudhibiti Tembo wanaoharibu mazao na kujeruhi wananchi Kata za Mindu, Kahulu na Tinginya -Tunduru?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Wananchi wanaoishi katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Tunduru na Namtumbo wamekumbwa na taharuki kubwa sana wakati wote wa maisha yao kuhusiana na hali halisi ya wingi wa tembo na uharibifu mkubwa unaofanyika, tembo wamefikia hatua ya kufika mpaka majumbani.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwavuna hawa tembo ili waweze kupungua na adha inayowakuta wananchi hawa ipungue? Ahsante. (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jacqueline Msongozi Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la fidia Mheshimiwa Mbunge nimtoe wasiwasi na Wabunge wengine wote. Jana tulikuwa na semina tuliweza kuliongelea hili suala, tulichofanya sisi kama Serikali tumekubaliana na mawazo ya Waheshimiwa Wabunge kwamba tunayachukua kwa umoja wao, tunaenda kuangalia sheria ambayo ilipitisha mwanzo kiwango hicho tuifanyie review kisha tutaleta humu humu Bungeni tuone namna iliyobora ya kuangalia thamani ya hawa wananchi ambao wanapata hasara ya kupoteza mazao na wengine wanapoteza hadi maisha ili angalau hii fidia au kifuta machozi na jasho kiweze kukidhi haja ya wananchi.

Mheshimiwa Spika, suala lingine la kuhusu taharuki ya tembo, ni kweli hii ni changamoto kubwa na tunawapa pole sana wananchi ambao wamekuwa wakikumbana na changamoto hii ya wanyama wakali hususan tembo. Serikali ina mkakati mahsusi wa kuhakikisha kwamba tunaanzisha vituo viwe karibu sana na maeneo yaliyohifadhiwa ili angalau taharuki hii inapojitokeza basi Askari wawe karibu kutatua tatizo hili.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo tumeendelea kutoa elimu kwa wananchi ili tuwe na ushirikishwaji wa karibu na jamii ili kudhibiti hawa wanyama wakali na waharibifu. Ahsante. (Makofi)