Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuhakikisha Maporomoko ya Kalambo yanatangazwa ili yawe na mchango wa kiuchumi kwa Taifa?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kwa Serikali.

Mheshimiwa Spika, maporomoko ya Kalambo ni miongoni mwa vivutio vilivyo Kusini Nyanda za Juu na ni ukweli usiopingika kwamba maporomoko haya kuachiwa chini ya TFS ambayo siyo kazi yake ya kutangaza vivutio vya kitalii ni kukosesha Taifa hili mapato sahihi.

Je, Serikali iko tayari kuyaondoa maporomoko haya kuwa chini ya umiliki wa TFS na kupeleka katika taasisi ambayo kazi yake mahsusi ni kwa ajili ya kutangaza vivutio vya utalii?

Swali la pili, kwa sababu kutangaza ni pamoja na uwepo wa bajeti na Wizara bado haijaleta bajeti yake. Je, watatuhakikishia kwamba kama maporomoko haya yataendelea kuwa chini ya TFS bajeti yake itaonekana ambayo iko mahsusi kwa ajili ya kutangaza vivutio vya utalii?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kandege, Mbunge wa Kalambo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kuyapeleka haya maporomoko haya maporomoko katika taasisi ya TFS tuliona kuna mbinu nyingine ambazo zinahitaji kusimamiwa na taasisi hii ya huduma za misitu Tanzania. Kwanza, kuna misitu ndani yake lakini pia kuna uoto wa asili ambao ndani yake unatunza vyanzo vya maji, hivyo TFS ni sahihi kabisa kusimamia maporomoko haya.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo taasisi zilizoko chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii zote zinatangaza masuala ya utalii. Tumeanza kujenga miundombinu ya barabara katika eneo hilo, pia tumetengeneza ngazi za kufika chini, tunatarajia pia kuanzisha masuala ya cable car katika maporomoko hayo ambayo tunatarajia kwamba tutapata watalii wengi sana ambao watakuwa wanatoka nchi jirani na ndani ya nchi.

Sambamba na hilo, tunajenga daraja ambalo litaunganisha Zambia na Tanzania, hii yote ni mikakati ambayo imepangwa ndani ya bajeti ya TFS. Kwa hiyo nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba tunaenda kufanya mambo mazuri na Kalambo inaenda kufunguka. Ahsante.