Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 30 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 264 2022-05-25

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:-

Je, ni lini barabara inayotoka Karagwe kupitia Nkwenda hadi Murongo itatengenezwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY KASEKENYA MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Lwehikila Theonest, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, zabuni kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Kyerwa hadi Chonyonyo (Kilometa 50) zimetangazwa na kufunguliwa tarehe 10 Mei, 2022. Kwa sehemu iliyobaki, Serikali ipo kwenye hatua ya manunuzi ya kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hiyo, ahsante.