Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 30 Energy and Minerals Wizara ya Madini 263 2022-05-25

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itawawezesha wachimbaji wadogo kwa kuwapatia mikopo katika Wilaya ya Mbogwe?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nicodemas Henry Maganga, Mbunge wa Jimbo la Mbogwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo mwanzo Serikali ilikuwa na utaratibu wa kuwapatia mikopo wachimbaji wadogo kwa lengo la kuwaongezea mitaji ili kuwafanya wafanye shughuli zao kwa tija. Baadaye tathmini ilifanyika na ilionesha upotevu wa fedha hizo. Kufuatia tathmini hiyo, Serikali inaendelea kuangalia namna bora ya kuwapatia mikopo wachimbaji wadogo nchini wakiwemo wa Wilaya ya Mbogwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hatua hiyo, Serikali kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limeingia makubaliano (MoU) na Benki za CRDB, NMB na KCB kwa ajili ya kuwapatia mikopo wachimbaji wadogo.