Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 28 Water and Irrigation Wizara ya Maji 242 2022-05-23

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza:-

Je, ni lini mradi wa maji mserereko wa Kiburubutu Ifakara utakamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abubakari Damian Asenga, Mbunge wa Jimbo la Kilombero, kama ifutavyo:-

Mheshimiwa Spika, mradi wa maji wa Mserereko wa Kiburubutu ni miongoni mwa miradi itakayotekelezwa kupitia mradi wa Miji 28 ikiwemo mji wa Ifakara. Ujenzi wa mradi huo utaanza kabla ya kumalizika kwa mwaka huu wa fedha 2021/2022.