Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 57 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 760 2023-06-28

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itawachukulia hatua viongozi wa Vyama vya Msingi waliodhulumu fedha za wakulima wa kahawa Mbozi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa George Ranwell Mwenisongole, Mbunge wa Jimbo la Mbozi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya uchunguzi kwa Vyama vya Ushirika 20 vilivyopo Wilayani Mbozi ambapo kati ya hivyo, vyama nane vimekutwa na changamoto mbalimbali ikiwemo wakulima kupunjwa malipo ya mauzo ya kahawa; vyama kutowasilisha makato ya ushuru kwa Halmashauri na watoa huduma; na kampuni ya ununuzi wa kahawa kushindwa kulipa fedha za mauzo ya kahawa.

Mheshimiwa Spika, hatua za stahiki zimechukuliwa kwa viongozi na watendaji waliobainika kuhusika na ubadhirifu uliojitokeza. Hatua hizo ni pamoja na kuondolewa kwa viongozi katika nafasi zao; kufanya uchaguzi wa bodi za mpito; na kampuni ya Taylorwinch kulipa kiasi cha shilingi 26,978,094 iliyokuwa inadaiwa na Chama cha Ushirika cha Isaiso. Vilevile taarifa za uchunguzi kwa Vyama vya Ushirika 20 ziliwasilishwa katika Ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Songwe kwa ajili ya mapitio na kuchukua hatua kwenye maeneo yenye viashiria vya rushwa, wizi na ubadhirifu.