Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 57 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 753 2023-06-28

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: -

Je, kuna maamuzi mengine baada ya Kamati ya Mawaziri nane kurudisha kwa wananchi wa Itigi shamba la Kampuni ya Tanganyika Packers?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, shamba la iliyokuwa Kampuni ya Tanganyika Packers ni kituo cha kupumzishia mifugo kinachojulikana kwa jina la Kitaraka Holding Ground. Shamba hili linamilikiwa na Serikali tangu tarehe 1 Mei, 1955 na linatambulika kwa Na. 35 na Hati ya Kumiliki Ardhi Na. 15467 inayotaja ukubwa wa shamba kuwa ni ekari 45,000 (hekta 18,218.623) kwa ajili ya malisho na kutunzia mifugo (cattle holding ground).

Mheshimiwa Spika, Kamati ya Mawaziri nane wa kisekta ya kutatua migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975 haijarudisha kwa wananchi wa Itigi shamba la iliyokuwa Kampuni ya Tanganyika Packers. Serikali imeelekeza ifanyike tathmini ya kina ya shamba la Kitaraka ili kubaini hali halisi kwa sasa kwa ajili ya kuwezesha Serikali kufanya uamuzi wa kumaliza mgogoro uliopo.