Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 57 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 750 2023-06-28

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu kuhusu hewa ya ukaa ili wananchi waelewe na wanufaike na elimu hiyo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, biashara ya kaboni (biashara ya hewa ukaa) ni moja ya mbinu za kupunguza uzalishaji wa gesijoto (mitigation) ambayo iliridhiwa katika Itifaki ya Kyoto ikizitaka nchi wanachama kupunguza uzalishaji wa gesijoto iliyorundikana angani. Biashara hii ipo katika masoko ya aina mbili ambayo ni Soko la Hiari/Huria (Voluntary Carbon Market) na Soko la Umoja wa Mataifa (Official Carbon Market).

Mheshimiwa Spika, Serikali imeandaa Mwongozo wa Biashara ya Kaboni pamoja na Kanuni zake za mwaka 2022. Aidha, elimu kuhusu biashara ya kaboni hadi sasa imetolewa kimakundi ikiwemo, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira, Wizara zote za kisekta pamoja na taasisi zake, Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya wote, Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mkoa na kwa wadau mbalimbali. Aidha, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kutoa elimu ya mazingira kwa Umma ikiwemo ya biashara ya kaboni.

Mheshimiwa Spika, ni matumaini ya Serikali kwamba kupitia jitihada hizo wananchi watapata uelewa na kunufaika na biashara ya kaboni. Nakushukuru.