Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 52 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 693 2023-06-21

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kufanya mapitio sheria ya Manunuzi ya umma kwa kuwa ni kikwazo kwa utekelezaji wa miradi katika Halmashauri?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango, imefanya mapitio ya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura 410 na kuandaa mapendekezo ya kutunga upya sheria hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mapendekezo hayo yamekamilika na muswada wa kutunga upya sheria ya ununuzi wa umma unatarajiwa kuwasilishwa Bungeni kwa ajili ya kusomwa kwa mara ya kwanza katika Mkutano wa Kumi na Moja wa Bunge la Kumi na Mbili.