Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 52 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 692 2023-06-21

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaweka Kituo kidogo cha Forodha katika Kata ya Itiryo – Bikonge Tarime Vijijini?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Mwikwabe Waitara, Mbunge wa Tarime Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania imeanza utekelezaji wa Mpango wa Miaka Mitano (2022/2023 – 2026/2027) wa ujenzi wa nyumba za wafanyakazi na ofisi katika maeneo yote yaliyobainishwa kupitia utafiti wa mwaka 2021/2022 kuhusu mahitaji ya ofisi za TRA nchini. Mpango huo umejumuisha Mkoa wa Mara na utekelezaji umeanza katika ujenzi wa nyumba mbili za wafanyakazi na usanifu wa ujenzi wa Ofisi ya Forodha mpakani Kilongwe – Rorya. Aidha, usanifu wa ujenzi wa majengo ya nyumba za watumishi mpakani Sirari umekamilika na ujenzi utaanza mapema baada ya kumpata mzabuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji katika vituo vingine vya Mkoa wa Mara utaanza kadri ya upatikanaji wa fedha, ikiwa ni pamoja na Kogaja, Borega, Kirumi na Itiryo – Bikonge.