Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 684 2023-06-21

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI K.n.y. MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza eneo la ekari 1000 za Shirika la Elimu Kibaha?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEORGRATIUS J. NDEJEMBI) aliuliza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silyvestry Francis Koka, Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Elimu Kibaha lina eneo lenye ukubwa wa hekta 1,358 katika Mji wa Kibaha. Eneo lenye ukubwa wa hekta 675.31 limeendelezwa kwa huduma mbalimbali zinazotolewa na Shirika. Aidha, eneo lenye ukubwa wa hekta 220.1 limetengwa kwa ajili ya upanuzi wa huduma za Shirika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lenye ukubwa wa hekta 170.913 limetengwa kwa ajili ya kuanzisha shamba darasa la kilimo cha umwagiliaji (block farming). Aidha, Shirika limetenga eneo lenye ukubwa wa hekta 38.84 kwa ajili ya uwekezaji (investment hub) lililopo mkabala na barabara ya Morogoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lililobaki lenye ukubwa wa hekta 252.837 linatumika kwa ajili ya huduma nyingine za kijamii ikiwemo Makanisa na Misikiti na lina miundombinu ya umeme, maji na limepitiwa na bomba la mafuta (TAZAMA).