Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 33 Enviroment Wizara ya Maliasili na Utalii 274 2016-05-31

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:-
Je, Serikali ina uhakika gani na usalama wa nchi yetu katika mpaka wa Pori la Akiba la Kimisi na Burigi na Mto Kagera?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Constatine John Kanyasu Mbunge wa Geita Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu inaendelea kuimarisha ulinzi wa rasilimali za wanyamapori zilizopo ndani ya Mapori ya Akiba yakiwemo ya Kimisi na Burigi katika kukidhi malengo ya uhifadhi endelevu kwa maslahi ya Taifa. Hii ni pamoja na kupambana na uvamizi wa mifugo, shughuli za kilimo, uharibifu wa mazingira na ujangili ndani ya hifadhi hizo. Aidha, pamoja na ulinzi wa ndani ya hifadhi, eneo la mpaka wa Mto Kagera na Pori la Akiba la Kimisi na Burigi limeonesha kuwa na changamoto zaidi zikiwemo za uhamiaji haramu na uingizaji wa silaha ambazo zinatumika kwa ujangili na ujambazi hivyo kulifanya eneo hilo la mpakani kuhitaji ulinzi zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu imekuwa ikishirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama ngazi za Wilaya na Mkoa, kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi kwa upana wake katika eneo hii mpakani.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu itaendelea kuimarisha doria ndani ya mapori ili kuboresha uhifadhi wa wanyamapori na kuhakikisha usalama katika maeneo hayo. Aidha, wavamizi wa hifadhi kwa shughuli za mifugo wanaweza kutumiwa kuhatarisha usalama wa nchi. Hivyo tunatoa rai kwa wananchi na wadau wengine kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali katika dhana nzima ya ulinzi shirikishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama itaendelea kuimarisha ushirikiano na nchi jirani kuhakikisha ulinzi na usalama wa mipakani unakuwa madhubuti ili kudhibiti madhara yanayotokana na uvamizi wa mifugo na wahamiaji haramu.