Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 3 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 37 2016-09-08

Name

Omary Ahmad Badwel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. OMARY A. BADWEL aliuliza:-
Wananchi wanaoishi kwenye maeneo yenye rasilimali mawe, mchanga na maji inapotokea wakandarasi wanachukua rasilimali hizo au mojawapo kwa ajili ya ujenzi huchukua bure au kwa malipo kidogo na hivyo kuwakosesha wananchi haki ya kunufaika na rasilimali hizo; hali hii ni tofauti na maeneo yenye madini ambapo wananchi hunufaika na uwepo wake:-
Je, Serikali haioni haja ya kuweka bei elekezi kwa wakandarasi wanaohitaji mawe, mchanga au maji ili wananchi wanaoishi maeneo yenye rasilimali hizo waweze kunufaika?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omary Ahmad Badwel, Mbunge wa Bahi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Sheria ya Madini ya mwaka 2010 na kanuni zake inamtaka kila mmiliki wa eneo la kuchimba madini amiliki leseni halali kutoka Wizara ya Nishati na Madini, hata hivyo leseni katika maeneo ya uchimbaji wa madini ya viwanda na ujenzi yanatakiwa pia kupata leseni bila kuchimba kiholela. Wakandarasi wanaofanya kazi ya ujenzi hulazimika pia kupata leseni za kuchimba madini ya ujenzi na kulipa mrabaha pamoja na ada nyingine kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Spika, kwa wakandarasi wasiokuwa na leseni za uchimbaji hununua madini ya ujenzi kwa wananchi wanaochimba na pia kufanya shughuli za ujenzi, pamoja na hayo, Wizara kwa kushirikiana na Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMA) hutoa matangazo kwenye Ofisi za Madini za Kanda na Maafisa Madini Wakazi yakionesha bei ya soko ya ndani ya ujenzi.
Mheshimiwa Spika, wachimbaji wa madini ya ujenzi wanaweza kuwasiliana na ofisi ya madini kupata mwongozo wa bei ya soko kwa sasa ili kupata ufahamu wa bei halisi ya mazao hayo.