Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 140 2023-09-08

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: -

Je, lini Serikali itafanya marekebisho ya sheria zisizo rafiki kwa wavuvi nchini?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/2024 Serikali imepanga kuendelea kupitia na kufanya marekebisho ya Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya mwaka 2003 ili kukidhi mahitaji ya hali halisi ya sasa ya shughuli za uvuvi. Aidha, Serikali ina utaratibu wa kufanya maboresho ya kanuni mbalimbali za uvuvi mara kwa mara ili kuondoa kero na kuboresha mazingira ya biashara kwa wadau wa uvuvi. Kwa mfano, katika mwaka 2019 Serikali ilirekebisha kanuni kuruhusu leseni ya uvuvi iliyokatwa kwenye Wilaya moja kutumika katika Wilaya zote katika ziwa husika au ukanda wote wa bahari. Pia mwaka 2020 Serikali ilirejelea kanuni za uvuvi kuruhusu ongezeko la kina cha nyavu za makila katika Ziwa Victoria kutoka macho 26 mpaka macho 78 kwa uvuvi wa samaki aina ya sangara.

Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea na tathmini ya sheria, kanuni, na miongozo iliyopo katika sekta ya uvuvi ili kubaini sheria zisizo rafiki kwa wavuvi nchini na kuzifuta au kuzirekebisha. Aidha, Wizara yangu iko tayari kupokea maoni na ushauri wa wadau mbalimbali wakiwemo Waheshimiwa Wabunge juu ya sheria zetu zinazohitaji kufanyiwa maboresho, naomba kuwasilisha.