Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Finance Wizara ya Fedha 128 2023-09-08

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza:-

Je, kwa kodi ya mapato kwa wachimbaji wadogo wa madini isiunganishwe na Mineral Market Management Information System (MMMIS)?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwanza niwapongeze sana Taifa Stars jana kwa kutuandikia historia kubwa sana. Kiongozi akiwa na baraka malango yote yanafanyika, kila linalofanyika kwa sababu ya baraka za Mama Samia linakubali tu ndiyo maana hata Yanga tukaingia makundi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo ya awali, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Jonathani Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kufuatia maelekezo ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuzitaka taasisi za umma kuhakikisha mifumo yote ya mapato na matumizi inasomana, Mamlaka ya Mapato Tanzania inaendelea kuunganisha na kufungamanisha mifumo yake ya usimamizi wa mapato na mifumo ya taasisi nyingine ikiwemo mifumo ya Mineral Market Management Information System.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Mamlaka ya Mapato Tanzania na Tume ya Madini zimeingia makubaliano ya kubadilishana taarifa ili kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato ya kodi na yasiyo ya kodi. Aidha, kodi ya mapato kwa wachimbaji wadogo wa madini inakusanywa katika masoko ya madini chini ya usimamizi wa Tume ya madini kwa niaba ya Mamlaka ya Mapato Tanzania.