Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 127 2023-09-08

Name

Amina Ali Mzee

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR K.n.y. MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa madarasa na mabweni ya Chuo cha Usafirishaji (NIT) Mabibo?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Ali Mzee, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali kupitia East Africa Skills for Transformation and Regional Integration Project (EASTRIP), mradi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia, imeanza ujenzi wa mabweni mawili yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 1,500. Ujenzi wa mabweni hayo umefikia asilimia 28. Aidha, kupitia mradi huo Serikali inajenga jengo lenye Madarasa ya wanafunzi 1,500 pamoja na maabara na karakana yenye kuchukua wanafunzi 500 kwa wakati mmoja ambapo ujenzi huo umefikia asilimia 30.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Rasilimali Mafunzo (maktaba) chenye madarasa yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 1,653 kwa wakati mmoja ambapo ujenzi huo kwa sasa upo kwenye asilimia 85.

Aidha, katika mwaka wa fedha 2023/24, Serikali kupitia mapato ya ndani ya Chuo, itaanza ujenzi wa Jengo la Kitaaluma la ghorofa tano litakalokuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 4,700 kwa siku, mara litakapokamilika.