Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 119 2023-09-07

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:-

Je, lipi tamko la Serikali kwa watuhumiwa waliopo magereza ya nchi za nje wanaomiliki vitambulisho na hati za kusafiria za Tanzania?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fakharia Shomari Khamis, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Pasipoti na Hati za Kusafiria, Sura ya 42, pasipoti hutolewa kwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa madhumuni ya kusafiria nje ya nchi. Pale inapothibitika kuwa raia wa nchi za nje wanamiliki hati za kusafiria za Tanzania kinyume na matakwa ya sheria yetu ya pasipoti wanakuwa wametenda makosa na hivyo wanastahili kuchukuliwa hatua za kisheria.

Mheshimiwa Spika, naomba kutumia fursa hii kumshauri Mheshimiwa Mbunge kama ana taarifa zitakazowezesha kupatikana kwa watuhumiwa hao azikabidhi kwa vyombo vyetu ili waweze kuchukuliwa hatua stahiki, nashukuru.