Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 91 2023-09-05

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:-

Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa nyumba za makazi ya polisi Moshi Manispaa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI, MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuena Athumani Bushiri, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tathmini kwa ajili ya ukarabati wa nyumba 147 za makazi ya askari polisi zilizoko Manispaa ya Moshi imeonesha kuwa kiasi cha shilingi bilioni 3.6 zinahitajika. Fedha hizo zinatarajika kutengwa kwa awamu kuanzia kwenye Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2024/2025 ambapo ukarabati wa nyumba 15 unatarajiwa kuanza kutekelezwa, nakushukuru. (Makofi)