Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 90 2023-09-05

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:-

Je, lini Kituo cha Polisi Bububu pamoja na nyumba za Askari vitafanyiwa ukarabati?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantakaje Haji Juma, Mbunge wa Jimbo la Bububu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imepanga kukarabati Kituo cha Polisi cha Bububu kwa awamu. Kwa awamu ya kwanza Serikali inakarabati hanga la kuishi familia 18 za askari ambalo linagharimu shilingi 19,358,450 na kwa sasa umefikia katika hatua ya umaliziaji. Baada ya awamu hii, Serikali imepanga kutumia shilingi 46,000,000 kukarabati kituo hicho pamoja na nyumba za askari katika mwaka wa fedha 2024/2025, nakushukuru.