Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 87 2023-09-05

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa mradi wa lambo Kata ya Nsimbo, Kijiji cha Mwenge, Halmashauri ya Nsimbo?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Jimbo la Nsimbo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuongeza upatikanaji wa maji kwa ajili ya mifugo hapa nchini, Serikali ilianza ujenzi wa mabwawa manne ya maji kwa mifugo likiwemo bwawa la Isulamilomo lililopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo. Aidha, ujenzi wa Bwawa la Isulamilomo haukukamilika katika muda uliopangwa kutokana na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa mradi, ikiwemo kukosekana kwa barabara ya kusafirisha mitambo kwenda eneo la mradi na kipindi kirefu cha mvua nyingi katika eneo la mradi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na changamoto hizo, Mkandarasi aliomba kuongezewa muda wa kukamilisha ujenzi wa bwawa hilo ambapo ujenzi unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba, 2023. Kwa sasa, Mkandarasi yupo katika eneo la mradi akiendelea na kazi ya ujenzi wa tuta na njia ya utoro wa maji. Naomba kuwasilisha.