Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 80 2023-09-05

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza:-

Je, ni minara mingapi ya mawasiliano ya simu itasimikwa Uyui kati ya minara 780 itakayojengwa nchi nzima?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Athuman Almas Maige, Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mradi wa Tanzania ya Kidijitali (DTP), Serikali imeainisha kata tisa zilizopo Uyuyi ambazo zimepatiwa watoa huduma (Airtel, Halotel na TTCL) hivyo kufanya idadi ya minara tisa itakayojengwa na tunatarajia vijiji 26 vilivyopo katika kata hizo vitanufaika na huduma baada ya kukamilika kwa ujenzi wa minara hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Wilaya ya Uyui ni miongoni mwa Wilaya zinazonufaika na Miradi ya Mawasiliano kupitia UCSAF, ambapo idadi ya minara 28 imejengwa na imekamilika katika kata 25 zilizopo wilayani humo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuboresha na kuimarisha upatikanaji wa huduma kwa upande wa Jimbo la Tabora Kaskazini, Kata za Igulungu, Kalola, Ufuluma, Nsimbo na Upuge zimefanyiwa tathmini na sasa Serikali kupitia UCSAF inamtafuta mtoa huduma atakayefikisha huduma ya mawasiliano katika maeneo hayo.