Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 79 2023-09-05

Name

Simai Hassan Sadiki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa dharura wa kunusuru athari za mabadiliko ya tabianchi - Nungwi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) naomba kujibu swali la Mheshimiwa Simai Hassan Sadiki, Mbunge wa Jimbo la Nungwi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua changamoto za athari za mabadiliko ya tabianchi zilizopo eneo la Nungwi. Tayari, Serikali kupita Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 imetenga kiasi cha shilingi milioni 650 kwa ajili ya kufanya tathmini ya awali ya kuzuia athari hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Hatua hizo ni pamoja na kuelimisha wananchi kupanda mikoko pamoja na kuhamasisha ulimaji wa mwani usioharibu fukwe. Serikali zote mbili za JMT na SMZ zitashirikiana katika kutafuta fedha zaidi ili kudhibiti uharibifu unaotokea eneo la Nungwi, nakushukuru.