Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 76 2023-09-05

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:-

Je, lini Kituo cha Afya Kata ya Kafita na Zahanati ya Kijiji cha Nyijundu zitafunguliwa na kupelekewa vifaa baada ya ujenzi kukamilika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Nassor Amar, Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilitenga bajeti ya shilingi milioni 500 katika mwaka wa fedha 2020/2021 kwa ajili ya ujenzi katika Zahanati ya Nyijundu ambayo imepandishwa hadhi kuwa kituo cha afya. Ujenzi huo umekamilika na vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 120.4 vimepelekwa na huduma zimeanza kutolewa mwezi Aprili, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa Kituo cha Afya Kafita unaendelea kwa fedha za TASAF shilingi milioni 500 ambapo majengo yanayojengwa ni jengo la kuhudumia wagonjwa wa nje, jengo la maabara, jengo la wodi ya wazazi na jengo la upasuaji. Aidha, ujenzi wa jengo la kuhudumia wagonjwa wa nje na maabara umekamilika na vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 120.4 vimepelekwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri inaendelea na taratibu za ukamilishaji wa majengo yaliyobakia na huduma za awali zitaanza kutolewa kwenye majengo yaliyokamilika ifikapo mwezi Octoba mwaka 2023, ahsante.