Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 75 2023-09-05

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa mabweni yaliyoanzishwa na wananchi kwa michango yao katika shule za kata nchini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Regina Ndege Qwaray, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023, Serikali iliidhinisha kiasi cha shilingi bilioni 9.21 kwa ajili ya ukamilishaji wa mabweni 461, kati ya hayo mabweni 28 ni kwa ajili ya shule za msingi zenye wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka 2023/2024 Serikali imetenga kiasi cha shilingi milioni 200 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa mabweni ili kuunga jitihada zilizofanywa na wananchi za kujiletea maendeleo. Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya mabweni kila mwaka kadiri ya upatikanaji wa fedha.