Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 68 2023-09-04

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO K.n.y. MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza ujenzi wa Kituo cha Polisi Turiani kilichojengwa kwa nguvu za wananchi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jonas Van Zeeland, Mbunge wa Mvomero kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa kupitia michango mbalimbali ya wananchi inayofikia shilingi milioni 36, Kituo cha Polisi Turiani kimefikia hatua ya lenta. Katika mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali imepanga kutumia fedha toka Mfuko wa Tuzo na Tozo ili kuendeleza ujenzi wa kituo hicho ambacho hadi kukamilika kitakuwa kimegharimu shilingi milioni 110, ahsante.