Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 5 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 62 2023-09-04

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatoa elimu kwa wafugaji kuhusu matumizi ya biogas ili kuhamasisha ufugaji wa kisasa?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekuwa ikitoa elimu ya ufugaji bora ikiwa ni pamoja na matumizi ya samadi kuzalisha biogas ambayo ni nishati mbadala ya kupikia na rafiki kwa mazingira.

Mheshimiwa Spika, matumizi ya nishati mbadala ya biogas ambayo inatokana na kinyesi cha mifugo ikitumika vizuri, itapunguza matumizi ya kuni na mkaa hivyo kuboresha maisha ya wafugaji na kuhifadhi mazingira. Kutokana na umuhimu huo, Wizara kupitia Wakala ya Mafunzo ya Mifugo (LITA), inatoa mafunzo ya utengenezaji wa biogas kwa wanafunzi wanaosoma katika vyuo vyake katika ngazi ya cheti na diploma ili watakapohitimu masomo hayo, wawe na ujuzi wa teknolojia ya biogas na waweze kuwafundisha wafugaji matumizi sahihi ya teknolojia hiyo pia. LITA hutoa mafunzo ya muda mfupi kwa wafugaji au vikundi vya wafugaji vinavyohitaji mafunzo hayo katika kampasi za Mpwapwa na Tengeru.