Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 2 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 27 2016-09-07

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:-
Katika eneo la Ndolezi Wilaya ya Mbozi kuna kimondo ambacho ni cha aina yake katika nchi hii na dunia kwa ujumla:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhamasisha watalii wa ndani na nje ya nchi kuja kukiangalia Kimondo hicho ili kuchangia pato la taifa?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii napenda kujibu swali la Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga Mbunge wa Vwawa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubalina na Mheshimiwa Mbunge kuwa Kimondo hiki kilichopo Kusini Magharibi mwa Kilima cha Marengi, Kijiji cha Ndolezi Wilaya ya Mbozi, Mkoani Mbeya ni cha kipekee hapa nchini, na kwakweli na duniani kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kulingana na taarifa za kitaalamu kimondo hiki kinaaminika kuwa kati ya vimondo nane vikubwa zaidi duniani kikikadiriwa kuwa na uzito wa tani 12, urefu wa mita 3.3, upana wa mita 1.63 na kimo cha mita 1.22. Sehemu yake kubwa ni chuma ambayo asilimia 90.45 na sehemu iliyobaki inajumuisha nikeli asilimia 8.69, shaba asilmia 0.66, sulphur asilimia 0.01, fosfori asilimia 0.11. Kwa kuzingatia upekee na umuhimu wake, mwaka 1967 kilitangazwa kuwa Urithi wa Taifa kwa tangazo la Serikali Na. 90 la tarehe 1967. Taarifa kuhusinaa na tarehe na mwaka wa kuanguka kwa kimondo hiki bado haijulikani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu imeendelea kutangaza Kimondo cha Mbozi kama moja ya vivutio muhimu na adimu nchini na duniani. Uhamasishaji umefanyika kwa kutumia njia mbalimbali ndani na nje ya nchi, ikiwa ni pamoja na vipindi vya runinga vya zamadamu (Televisheni ya Taifa TBC1) na utalii wa ndani kupitia Kituo cha Channel Ten. Pia machapisho ya Tanzania; The Land of Great Heritage Sites na Tanzania Cultural Heritage Resources ambayo nakala zake pia husambazwa katika maonesho mbalimbali na balozi zetu nje ya nchi. Machapisho mengine ambayo hutolewa kwa Kiswahili ni pamoja na Jarida la Ifahamu Idara ya Mambo ya Kale na Jarida la Maliasili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maelezo na picha za kimondo hiki pia vimewekwa katikatovuti na mitandao mbalimbali duniani. Juhudi hizi pamoja na nyingine zimeendelea kuonesha matunda kwani takwimu zinaonesha kuongezeka kwa idadi ya watalii na mapato. Kwa mfano kati ya mwaka 2012/13 na 2014/2015 watalii waliongezeka kutoka jumla ya 990 hadi 1,681 na mapato kuongezeka kutoka Shilingi 811,000 hadi 2,426,000.