Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 5 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 55 2023-09-04

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG'WASI D. KAMANI aliuliza:-

Je, Serikali inatumia mfumo gani kuhakiki ubora na matokeo chanya ya programu mbalimbali zinazotolewa kwa vijana?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ng’wasi Kamani, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka mfumo wa ufuatiliaji na tathmini ya miradi na programu zote zinazotekelezwa ikiwemo programu za vijana. Katika kutekeleza hilo mwezi Januari, 2022 Serikali ilitoa Mwongozo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Miradi mbalimbali na Programu za Maendeleo. Kwa kuzingatia mwongozo huo, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu imekuwa ikifanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa programu mbalimbali kila robo mwaka. Aidha, Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu imekuwa ikifanya tafiti ili kupima matokeo ya utekelezaji wa programu mbalimbali, ikiwemo utafiti wa nguvu kazi ambao hufanyika kila baada ya miaka mitano.

Mheshimiwa Spika, matokeo ya utafiti wa nguvu kazi uliofanyika mwaka 2020/2021unaonesha kuwa kutokana na programu za vijana zinazotekelezwa ikiwemo Programu ya Kukuza Ujuzi, kiwango cha ujuzi cha juu kimeboreka. Kiwango cha ujuzi cha kati kimeongezeka kutoka asilimia 16.6 mwaka 2014 hadi kufikia asilimia 19.9 mwaka 2021, na kiwango cha ujuzi wa chini kimepungua kutoka asilimia 79.9 mwaka 2014 hadi asilimia 76.9 mwaka 2021.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali itaendelea kusimamia utekelezaji wa programu hizo ili ziweze kuleta tija kwa Taifa. Sambamba na hatua hiyo, mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali imepanga kufanya tathmini mahususi (tracer study) ya mafunzo yanayotolewa kupitia programu mbalimbali za kuwawezesha vijana kubaini mafanikio yaliyopatikana kwa kuwezesha kujiajiri na kuajiriwa, ahsante.