Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 4 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 51 2023-09-01

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawaendeleza wavuvi kwa kuanzisha uvuvi unaotumia dira maalum inayoelekeza samaki walipo?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) K.n.y WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amour Khamis Mbarouk, Mbunge wa Tumbe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara kupitia Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (Tanzania Fisheries Research Institute - TAFIRI), imeshaanza kuteleleza mradi wa kutambua maeneo yenye samaki yanayofaa kwa uvuvi (Potential Fishing Zones - PFZs) katika Bahari ya Hindi ili kuwasaidia wavuvi kujua maeneo yenye samaki wengi. Aidha, katika mradi huu, wavuvi wanawezeshwa kufanya uvuvi unaotumia dira maalum kwa kupewa taarifa za kijiografia (GPS) kupitia simu za mkononi ili kujua maeneo yenye samaki kwa wakati husika. Mradi huu wa majaribio ulifanyika kwa mafanikio kwa kushirikiana na wavuvi wa maeneo ya Mafia na Tanga kwa upande wa Tanzania Bara na Unguja na Pemba kwa upande wa Zanzibar.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa TAFIRI inatengeneza programu maalumu (mobile app) ambayo itawawezesha wavuvi kupata taarifa za maeneo ya uvuvi ambako samaki wanapatikana kwa wingi. Aidha, programu hiyo imekamilika kwa asilimia 90. Ahsante.