Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 49 2023-09-01

Name

Maida Hamad Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH aliuliza: -

Je, lini Serikali italipa madeni ya fedha za kusafirishia mizigo kwa Askari Wastaafu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maida Hamad Abdallah, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi limeshafanya uhakiki wa madeni ya kusafirisha mizigo ya askari polisi wastaafu 624. Uhakiki huo unaonesha kuwa jumla ya fedha zinazohitajika kwa ajili ya kusafirisha mizigo ya askari polisi wastaafu ni shilingi 806,067,788.02. Madai hayo yatalipwa baada ya Wizara ya Fedha kukamilisha taratibu za kuhamishia fedha hizo Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kukamilika. Ninakushukuru sana. (Makofi)