Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 3 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 44 2023-08-31

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji Kata za Kisorya, Igundu, Kwiramba, Namuhura, Butimba na Kasuguti - Mwibara?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Charles Muguta Kajege, Mbunge wa Mwibara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inaendelea na zoezi la kubaini maeneo yote yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji nchini ili kuyapima na kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili kupata sgharama halisi za kutekeleza miradi hii kabla ya kuanza ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Tume imejipanga kuyafikia maeneo mbalimbali yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji nchini ikiwemo maeneo yanayofaa kwa umwagiliaji yaliyopo ndani ya Jimbo la Mwibara ili kuingiza kwenye mpango wa utekelezaji, nakushukuru.