Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Finance Wizara ya Fedha 39 2023-08-30

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: -

Je, Serikali ipo tayari kuandaa mazingira kuwezesha biashara kati ya China na Tanzania kufanyika kwa shilingi?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chusmi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika biashara za Kimataifa, wafanyabiashara wanao uhuru wa kutumia sarafu yoyote inayorahisisha biashara na inayokubalika na nchi nyingine kwa lengo la kupunguza gharama za miamala na muda.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itafanyia kazi jambo hili ili kuona ni nini kinapaswa kufanyika kuwezesha wafanyabiashara wa nchi ya China kukubali matumizi ya sarafu ya Tanzania, ahsante.