Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 38 2023-08-30

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga Mahakama katika Makao Makuu ya Tarafa za Nalasi, Lukumbule na Namasakata – Tunduru?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mahakama inaendelea na utekelezaji wa Mpango wa ujenzi wa Mahakama hizi ambapo Mahakama ya Mwanzo ya Nalasi inajengwa katika mwaka huu wa fedha 2023/2024 ikiwa ni sehemu ya Mahakama za Mwanzo 71 zitakazojengwa nchi nzima. Tayari Mshauri Mwelekezi ameanza kufanya kazi, na mradi unatarajiwa kuanza Oktoba, 2023 na kukamilika kabla ya Juni, 2024. Mahakama za Mwanzo za Lukumbule na Namasakata zitaingizwa kwenye mpango ujao wa miaka mitano sambamba na tarafa nyinginezo nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika bajeti ya mwaka huu wa fedha moja ya Mahakama za Wilaya zitakazojengwa ni Wilaya ya Tunduru, ahsante.