Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Community Development, Gender and Children Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum 37 2023-08-30

Name

Martha Nehemia Gwau

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA N. GWAU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za kuwahifadhi waliofanyiwa ukatili ikizingatiwa kuwa ukatili kwa watoto na wanawake umeongezeka?

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Nehemia Gwau, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mpango wa kuwahifadhi waliofanyiwa ukatili (kujenga nyumba za kuwahifadhi waliofanyiwa ukatili), Serikali imeandaa Mwongozo wa Uanzishaji na Uendeshaji wa Nyumba Salama wa Mwaka 2019, kwa ajili ya manusura wa vitendo vya ukatili pamoja na wahanga wa biashara haramu wa usafirishaji wa binadamu. Lengo ni kuweka mazingira wezeshi kwa uanzishaji huduma ya nyumba salama kwa manusura wa ukatili wa kijinsia na kwa watoto hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, Hadi kufikia June 2023 jumla ya nyumba salama 12 zimeanzishwa na kusajiliwa katika Mikoa ya Arusha, Kigoma, Kilimanjaro, Dar es Salaam na Mwanza. Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa sekta binafsi kuhakikisha upatikanaji endelevu wa huduma hii kwa mujibu wa Mwongozo wa mwaka 2019.