Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 36 2023-08-30

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza: -

Je, upi mpango wa kudhibiti wanyama wanaoharibu mazao na kugharimu maisha ya watu Kata za Naarami, Lokisale, Moita, Lepruko na Makuyuni?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Valentine Magige, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mwingiliano kati ya binadamu na wanyamapori umekuwepo kwa muda mrefu. Hata hivyo, miaka ya hivi karibuni mwingiliano huo umeongezeka na kusababisha madhara kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kuua mifugo na kuharibu mali za wananchi ikiwemo mazao na wakati mwingine kusababisha vifo au kujeruhi wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia kuwepo kwa changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu, Wizara imeandaa mpango wa kongoa shoroba katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo Kata za Naarami, Lokisale, Moita, Lepruko na Makuyuni. Aidha, Wizara imewaelekeza wananchi kuacha kuanzisha shughuli za kibinadamu kwenye mapito ya wanyamapori ili kuepuka madhara yanayotokana na wanyamapori hao.