Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 34 2023-08-30

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kuitumia Bahari kwa michezo mbalimbali ya majini ili kuongeza kipato cha wananchi wa Jimbo la Kawe?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Askofu Josephat Mathias Gwajima, Mbunge wa Kawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sera ya Maendeleo ya Michezo ya Taifa ya mwaka 1995, Ibara ya 7(i) hadi (vi), jukumu la ujenzi na uendelezaji wa miundombinu ya michezo ni jukumu la Serikali Kuu, Mamlaka ya Serikali za Mitaa pamoja na wadau wa sekta ya michezo zikiwemo taasisi, mashirika na watu binafsi. Hata hivyo, Wizara kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wako katika mkakati wa kuziendeleza fukwe za Kunduchi na Kigamboni katika Jiji la Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, lengo ni kukuza mchezo wa Soka la Ufukweni ambao tayari TFF wameshaanzisha Ligi yake ambayo ilianza tangu Tarehe 19/08/2023 na inafanyika kwa siku za Jumamosi na Jumapili katika fukwe za Koko, na jumla ya Timu 16 zinashiriki Ligi hiyo. Aidha, naomba niliarifu Bunge lako Tukufu kuwa mwezi Julai, 2023, Timu ya Taifa ya Soka la Ufukweni ilishiriki mashindano ya mchezo huo Barani Afrika yaliyofanyika Nchini Tunisia na kushika nafasi ya tatu, nyuma ya Morocco na Senegal.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninatoa rai kwa wadau wa michezo mingine kama Mitumbwi na Ngalawa, Kuogelea, Mpira wa Kikapu na Wavu kuwekeza katika michezo hii ya ufukweni na kuziendeleza fukwe tulizonazo ili kukidhi matakwa ya michezo yao, kwani pamoja na kuongeza kipato kwa wananchi, michezo hii pia inasaidia kuimarisha afya na kutoa burudani kwa wananchi.