Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 26 2023-08-30

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Choma - Ziba – Nkinga - Simbo - Puge utaanza kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Seif Khamis Said Gulamali, Mbunge wa Manonga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) tayari imeanza maandalizi kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami kwa barabara ya Choma – Ziba – Nkinga – Simbo – Puge yenye urefu wa kilometa 109 ambapo Mhandisi Mshauri kwa ajili ya kufanya kazi ya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina amepatikana na ameanza kazi tarehe 24 Agosti, 2023 na anatarajia kukamilisha mwishoni mwa mwezi Oktoba, 2024. Baada ya kazi ya usanifu kukamilika, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi. Ahsante.