Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 21 2023-08-30

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga stendi za mabasi katika Halmashauri za Mkoa wa Tanga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Mzamili Zodo, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia mpando wa uboreshaji wa Majiji na Manispaa Tanzania TSCP imejenga Stendi ya Kisasa katika Jiji la Tanga na Halmashauri ya Mji wa Korogwe zilizogharimu takribani kiasi cha Shilingi billioni 10.7, ujenzi wa stendi hizo umekamilika na zinatumika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 Serikali imetenga bajeti ya shilingi billioni 10.312 kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ya stendi katika halmashauri nchini. Aidha, Serikali itaendelea kujenga stendi za mabasi katika halmashauri kwa awamu kupitia programu mbalimbali kama, TACTIC, TSCP na vyanzo vingine yakiwemo mapato ya ndani ya halmashauri, ahsante. (Makofi)