Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 48 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 418 2016-06-22

Name

Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE (K.n.y. MHE. LUCY S. MAGERELI) aliuliza:-
Matatizo ya migogoro ya ardhi na mipango miji ni suala nyeti sana linalohitaji kutazamwa sana katika zama hizi; na hivi karibuni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi aligawa ramani za maeneo ya mitaa ya Jiji la Dar es Salaam lakini zoezi hilo halikufanikiwa kutokana na kukosa mkakati ulioambatana na matumizi ya ramani hizo:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha ramani hizo zinapatikana kwa nchi nzima ili kusaidia kuongoza matumizi ya ardhi katika miji mingi nchini?
(b) Waziri Mkuu aliyepita, Mheshimiwa Mizengo Pinda alisema, Serikali ingeuza Government Bond ili kupata fedha za kugharamia mradi huu. Je, agizo hilo limefikia hatua gani katika utekelezaji?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kujibu swali Na. 418 la Mheshimiwa Lucy Simon Magereli, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) yote kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Mipango Miji Na. 8 ya mwaka 2007, kifungu cha 21(1) kinaeleza kwamba mipango yote iliyoidhinishwa na Mkurugenzi wa Mipango Miji na Vijiji kwa maana ya Mipango Miji ya jumla (Master plan) na ile ya kina (michoro ya mipango miji) itahifadhiwa na mamlaka husika ya upangaji kwa maana ya Halmashauri ya Jiji, Manispaa, Miji na Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli matatizo ya migogoro ya ardhi na mipango miji ni suala nyeti sana linalohitaji kupatiwa mtazamo wa kipekee. Ni kweli hivi karibuni niligawa ramani za maeneo ya mitaa ya Jiji la Dar es Salaam na zoezi hilo lilifanyika kwa lengo la kuwawezesha viongozi wa ngazi za mitaa kushiriki kikamilifu katika udhibiti wa ujenzi holela na uvamizi wa maeneo ya umma, maeneo ya wazi na yale yaliyohifadhiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu ina jukumu la kuhakikisha kuwa michoro yote ya mipango miji iliyoidhinishwa na Wizara inatumiwa kwenye Ofisi za Makatibu Tawala wa Mikoa na nakala zake kupelekwa katika Halmashauri husika na mamlaka hizo zina jukumu la kuweka michoro hiyo hadharani ili umma uweze kuona na kulinda maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Serikali kuuza bond ili kupata fedha za kugharamia mradi huu, suala hili halijatekelezwa, badala yake kila Halmashauri inaelekezwa kutumia vyanzo vyake vya ndani vya mapato kwa kushirikiana na sekta binafsi. Hii ni kutokana na Sheria ya Mipango Miji inayotoa fursa kwa wamiliki binafsi wa ardhi kuandaa mipango ya matumizi kwa mujibu wa sheria.