Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 18 2023-08-29

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: -

Je, Serikali ina utaratibu gani wa kufanya mazoezi ya utayari katika uokozi wa ajali majini katika Kivuko cha Kivukoni – Kigamboni?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lina boti moja ya maokozi iliyopo katika Daraja la Mwalimu Nyerere iliyopo Ofisi ya Mkuu wa Zimamoto na Uokoaji Wilaya ya Kigamboni ambayo hutumika kwa ajili ya maokozi ya ajali za majini katika Bahari ya Hindi na kwenye fukwe zote za Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limeandaa na kutekeleza mkakati wa utoaji wa elimu na mazoezi katika Wilaya ya Kigamboni kwa kushirikiana na Ofisi ya kivuko cha Magogoni – Feri, Kigamboni Beach Management Unit (BMU) na wavuvi kwa ajili ya utayari wa huduma ya uokoaji wakati wa ajali za majini katika Kivuko cha Kigamboni na maeneo mengine ya jiji. Mkakati huo unatekelezwa pia kwenye sehemu zote zenye bahari kuu, maziwa makuu na mito ikiwemo Mkoa wa Pwani, Mara, Kagera, Geita, Kigoma na Mwanza, nashukuru.