Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 7 2023-08-29

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: -

Je, lini TANROADS Mkoa wa Mara wataondoa vigingi katika maeneo ya Wananchi baada ya kushindwa kulipa fidia?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi wa napenda kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, Mbunge wa Bunda Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, upana wa eneo la hifadhi ya barabara zinazosimamiwa na Wakala ya Barabara Tanzania upo kwa mujibu wa Sheria ya Barabara ya mwaka 1932 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 1962 na baadaye mwaka 1967 ambapo lilikuwa ni mita 22.5 kutoka katikati ya barabara kila upande. Aidha, Sheria mpya ya Barabara Na. 13 ya mwaka 2007 na kanuni zake za mwaka 2009, ziliongeza upana wa eneo la hifadhi ya barabara kutoka mita 22.5 hadi mita 30 kila upande kutoka katikati ya barabara.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa wananchi ambao wamo ndani ya nyongeza ya mita 7.5 kwa nchi nzima Serikali inaangalia upya nyongeza hii na itaandaa mapendekezo ya maeneo gani yabakie na nyongeza hii ya mita 7.5 ili fidia ilipwe na maeneo gani wananchi waruhusiwe kuendelea na shughuli zao. Ahsante.