Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 1 2023-08-29

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: -

Je, nini mpango wa Serikali kuhusu malalamiko ya wastaafu juu ya kikokotoo kinachotumika kupiga mahesabu na kulipa mafao?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo, Mbunge wa Moshi Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilitangaza matumizi ya kanuni mpya ya mafao (kikokotoo) ya pensheni kuanzia tarehe 1 Julai, 2022 kupitia Gazeti la Serikali Na. 357 Toleo la tarehe 20 Mei, 2022. Kanuni hiyo iliandaliwa kwa kuzingatia haja ya kuboresha na kuwianisha mafao ya wanachama na kuifanya Mifuko ya Pensheni kuwa endelevu.

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuendelea kuwaelimisha wananchi hususani waajiri na wanachama wa Mifuko ya Pensheni wakiwemo wastaafu kuhusu faida ya kanuni mpya ya mafao ya pensheni. Hivyo, Serikali kupitia Mifuko ya Pensheni na kwa kushirikiana na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) imejipanga na inaendelea kutoa elimu ya Kanuni hiyo. Hadi kufikia Tarehe 30 Juni, 2023, Mifuko iliweza kutoa elimu kwa jumla ya waajiri 5,580 kati ya waajiri 6,200 waliopangwa kufikiwa kipindi hicho. Aidha, wanachama 131,497 walifikiwa na mafunzo hayo. Mifuko itaendelea kutoa elimu kama sehemu ya majukumu yao ya kila siku, ahsante.