Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 52 2016-02-01

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:-
Wananchi wa Mtaa wa Katoma, Kata ya Kalawala Wilaya ya Geita wameathirika sana na shughuli za Mgodi wa geita Gold Mine (GGM) ambapo nyumba zimepata nyufa na kuanguka kutokana na mitetemo, milipuko ya mara kwa mara inayoletwa na kelele na vumbi linaloathiri afya za wananchi wa mtaa huo pamoja na vyanzo vya maji.
Je, ni lini wananchi hao wa Katoma watapewa fidia za mali zao ili waondoke katika eneo hilo jirani kupisha shughuli za Mgodi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Upendo Furaha Peneza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ili kupata ufumbuzi wa malalamiko ya wananchi wa Mtaa wa Katoma, Wizara imeunda Timu ya Wataalam kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini kama athari zinazodaiwa na wananchi wa Katoma za kusababisha nyufa kwenye nyumba zao zinatokana na shughuli za ulipuaji wa baruti zinazofanywa na Mgodi wa GGM (Geita Gold Mine).
Mheshimiwa Spika, Timu hiyo itakamilisha kazi yake tarehe 25 Februari, mwaka huu na iwapo itabainika kuwa athari zinazolalamikiwa na wananchi wa Katoma zinatokana na shughuli za ulipuaji wa baruti kwenye mgodi huo, basi Serikali itahakikisha kuwa Mgodi wa GGM unalipa fidia stahiki kwa wananchi hao ili wahame na kupisha shughuli za uchimbaji madini kwenye eneo hilo.