Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 14 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 180 2023-04-27

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA kwenye Vijiji 23 Wilayani Mkalama?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jesca David Kishoa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini, Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Pili, katika Wilaya ya Mkalama unatekelezwa na Mkandarasi CRJE – CTCE Consortium. Mradi unalenga kupeleka umeme katika vijiji vyote 25 vya Wilaya ya Mkalama ambavyo havina umeme na Mkandarasi yupo katika eneo la site akiendelea kuwasha umeme.

Mheshimiwa Spika, kwa ujumla, mradi huu wa kusambaza umeme katika Wilaya ya Mkalama unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Disemba, 2023, nakushukuru.