Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 51 2016-02-01

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE (K.n.y MHE. FRANK G. MWAKAJOKA) aliuliza:-
(a) Je, Serikali ina Mpango gani wa kugenga Kituo cha Polisi chenye hadhi ya Wilaya hapa Tunduma ili kuendana na ongezeko la watu na wageni wanaoingia nchini?
(b) Je, Serikali haioni vema ujenzi wa kituo hicho uende sambamba na ujenzi wa nyumba zenye gharama nafuu kwa Polisi wetu ambao wana shida kubwa ya makazi?
SPIKA: Sasa Mheshimiwa Silinde wewe Tunduma si ulishaondoka, majibu ya swali hilo Mheshimiwa Naibu, Waziri Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Hamad Yussuf Masauni. (Kicheko)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI YA WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Frank George Mwakajoka, Mbunge wa Tunduma, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa Kituo cha Polisi Tunduma ni kidogo na hakina nyumba za kutosha. Wilaya ya Momba inahitaji nyumba 150 ili kukidhi mahitaji ya makazi ya Askari. Kama ilivyo kwa maeneo mengi hapa nchini, changamoto kubwa ya ujenzi wa vituo vya Polisi na nyumba za askari ni uhaba wa fedha. Aidha, kwa Kituo cha Polisi Tunduma changamoto nyingine ni eneo la kufanya upanuzi wa kituo kilichopo sasa kwani kituo hicho kipo mpakani kando mwa barabara ya Sumbawanga.
Mheshimiwa Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha Jeshi la Polisi linaboreshewa makazi na kuwa na ofisi ili kuwezesha utoaji huduma kwa wananchi kuwa mzuri. Jeshi la Polisi chini ya utaratibu wa mikopo nafuu kutoka taasisi za kifedha za ndani na nje ya nchi lina mpango wa kujenga nyumba na ofisi za Polisi maeneo mbalimbali nchini. Kwa hivi sasa Serikali inakamilisha taratibu za kupata mkopo toka Bank ya Exim ya China ili kujenga nyumba 4,136 za makazi ya Askari katika Mikoa 17 hapa nchini.