Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 1 Water and Irrigation Wizara ya Maji 4 2016-09-06

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DANIEL E. MTUKA aliuliza:-
Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni imepata USD 17 milioni katika mgao wa USD 500 milioni zilizotolewa na Serikali ya India kusaidia miradi ya maji kwa bajeti ya 2016/2017.
Je, ni lini fedha hizo zitaanza kupelekwa katika Halmashauri husika ikizingatiwa kuwa shida ya maji imezidi kuwatesa wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni na kwingineko katika nchi yetu kwa ujumla?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Edward Mtuka, Mbunge wa Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, mwezi Julai, 2016, Serikali ya Tanzania na Serikali ya India zilifikia makubaliano ambapo Serikali ya India imekubali kuikopesha Tanzania mkopo wenye masharti nafuu wa dola za Marekani milioni 500 kwa ajili ya miradi ya maji. Mkopo huu utatekeleza miradi katika Miji 17 ikiwemo Mji wa Manyoni.
Mheshimiwa Spika, Miji mingine itakayofaidika na mkopo huu ni pamoja na Muheza, Mradi wa Maji wa Kitaifa wa Wanging‟ombe, Makambako, Kayanga, Karagwe, Songea, Zanzibar, Mradi wa Maji wa Kitaifa wa HTM, Njombe, Mugumu, Kilwa Masoko, Geita, Chunya, Mradi wa Maji wa Kitaifa wa Makonde, Sikonge, Kasulu na Rujewa.
Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa miradi ya maji chini ya mkopo huu itaanza mara baada ya kukamilisha taratibu za mkopo. Aidha, miradi hii itatekelezwa moja kwa moja na Wizara hivyo fedha hazitatumwa kwenye Miji au Halmashauri husika.