Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 6 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Rais TAMISEMI. 62 2016-02-02

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. SUSAN L. A. KIWANGA (K.n.y. MHE. OMARY T. MGUMBA) aliuliza:-
Vijana ndio nguvu kazi kubwa katika Taifa letu na Serikali haina uwezo wa kutoa ajira kwa vijana wote kwa sasa:-
(a) Je, Serikali itawawezesha kifedha vijana wa vijiji vyote 64 vya Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki katika makundi ili waweze kujiajiri wenyewe na kupunguza tatizo la ajira na umasikini wa vijana na akina mama?
(b) Je, ni lini Serikali itaanzisha kituo maalum cha kuwawezesha vijana kupata sehemu ya kujifunzia kwa vitendo shughuli mbalimbali za ujasiriamali na kupata taarifa mbalimbali za maendeleo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mgumba Tebweta Omary, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, lenye Sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, vijana katika Halmashauri ya Morogoro Kusini Mashariki, wamekuwa wakiwezeshwa kiuchumi kupitia fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Vijana ambapo kila Halmashauri hupaswa kutenga 5% ya mapato yake yandani kila mwaka wa fedha kwa ajili ya vijana. Katika bajeti ya mwaka 2014/2015 Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ilifanikiwa kutenga shilingi 10,300,000/= kwa vikundi vya vijana 19 kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali za kiuchumi. Aidha, katika bajeti ya mwaka 2015/2016 vikundi vya vijana vimetengewa Shilingi milioni 87,500,000 ili kuviwezesha kiuchumi na kujiajiri.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro imejenga Vituo viwili vya Mafunzo (Agricultural Resource Centres) katika Kata za Ngerengere na Mvuha kwa madhumuni ya kutoa elimu na mafunzo ya ujasiriamali ili kuwajengea vijana dhana ya uthubutu katika kufanya shughuli za kiuchumi.
Halmashauri imetoa mafunzo ya ufyatuaji wa matofali ya interlock kwa vikundi vya vijana katika Kata nne za Kinohe, Kisemu, Ngerengere na Mvuha, ambapo jumla ya vijana 40 wamewezeshwa kupata elimu hiyo ya ujasiriamali. Mpango huu ni endelevu na Halmashauri inakusudia kutenga fedha katika bajeti ya mwaka 2016/2017 kwa ajili ya ununuzi wa mashine ya kufyatulia tofali ili ziwezeshe kuwanufaisha vijana wengi zaidi kiuchumi na kuboresha maisha na makazi ya wananchi wa Wilaya hiyo.