Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 20 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 181 2022-05-11

Name

Salim Mussa Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gando

Primary Question

MHE. SALIM MUSSA OMAR aliuliza: -

Je, kuna Mwongozo unaosema kuwa Zanzibar Insurance Corporation haipaswi kushiriki kukata Bima za Miradi mikubwa?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y. WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Omar Salim, Mbunge wa Gando, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika la Bima la Zanzibar (Zanzibar Insurance Corporation) limesajiliwa kwa kupewa leseni Na. 00000821 na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) chini ya Sheria ya Bima Na. 10 ya Mwaka 2009. ZIC inafanya biashara za bima sehemu zote Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.

Mheshimiwa Naibu Spika, biashara ya bima nchini ni huria na inaendeshwa kwa jumla ya makampuni 31 ya bima ikiwemo ZIC. Aidha, kampuni zote zina haki sawa ya kutoa kinga ya majanga kwa miradi mbalimbali Tanzania Bara na Zanzibar. Hivyo, hakuna Mwongozo wowote unaokataza Zanzibar Insurance Corporation kushiriki katika biashara ya kukata bima za miradi mikubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa muktadha huo, Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC), kama ilivyo kwa kampuni nyingine yoyote ya bima iliyosajiliwa chini ya Sheria ya Bima Na. 10 ya Mwaka 2009, inaruhusiwa kuweka kinga ya bima kwa miradi mikubwa. Ahsante.